Msanii anayeitikisa Afrika kwa ngoma zake kali kama Azonto, Antenna na zinginezo, Fuse ODG ambaye alikuwa kwenye kipengele cha Best International Act: Africa kwenye Tuzo za BET 2015 aligoma kuhudhuria tukio hilo lililofanyika jana.
Akifunguka kupitia mtandao wa Twitter, Fuse ODG alisema wasanii wa Afrika wanafanyiwa dharau na kituo hicho cha TV ambacho ndio kimeandaa Tuzo hizo. Hii hapa tweet yake akiwafungukia kwanini hakutokea kwenye tukio lile.
Akifunguka kupitia mtandao wa Twitter, Fuse ODG alisema wasanii wa Afrika wanafanyiwa dharau na kituo hicho cha TV ambacho ndio kimeandaa Tuzo hizo. Hii hapa tweet yake akiwafungukia kwanini hakutokea kwenye tukio lile.
Dear @BET, the reason why I didn't come is because you give our awards backstage! You have no respect for our hard work and achievements
— Fuse ODG (@FuseODG) June 28, 2015
Mwaka jana ambapo tuzo hiyo ilichukuliwa na Davido, msanii wa Bongo flava, Diamond alilalamikia kitu hicho hicho ambacho Fuse ODG anakilalamikia sasa! Tatizo kubwa ni kwamba ugawaji wa Tuzo hizo kwenye kipengele hicho hufanyika asubuhi huku ukumbi ukiwa mtupu wakati tukio lenyewe linafanyika jioni.