Mtalam III Mtalam III Author
Title: Diamond apata shavu, kutumbuiza jukwaa moja na Iyanya, Yemi Alade, Olamide na wengine nchini Nigeria
Author: Mtalam III
Rating 5 of 5 Des:
Lengo la kufanya kila awezalo ili kulishika soko la Nigeria na Afrika kwa ujumla la mkali wa Bongoflava, Diamond lilishatimiaga zamani san...
Lengo la kufanya kila awezalo ili kulishika soko la Nigeria na Afrika kwa ujumla la mkali wa Bongoflava, Diamond lilishatimiaga zamani sana. Sasa hivi msanii huyo ni moja kati ya wasanii wanaokubalika sana Afrika.

Diamond anawania vipengele vitatu kwenye tuzo za MTV zijulikanazo kama MAMA, na pia bado wimbo wake ambao amemshikisha mkali kutoka Nigeria, Mr Flavour, ‘Nana’ unaendelea kufanya vizuri sana kwenye vituo mbalimbali vya TV hapa Afrika.

Diamond ambaye yuko nchini Nigeria akifanya media tour ya kuitangaza single yake mpya ‘Nana’, anatarajiwa pia kutumbuiza kwenye show ya MTV Road to MAMA itakayofanyika Ijumaa hii July 3, jijini Lagos.

Diamond ataungana na wasanii wa Nigeria akiwemo Iyanya ambaye ameshafanya naye collabo, Yemi Alade, Phyno, Olamide na wengine..

Author

Advertisement

 
Top